Friday, December 16, 2016

WAZIRI ATOA AGIZO JIPYA KWA MACHINGA#johnleo

Waziri wa TAMISEMI George Simbachawene amewataka wamachinga kutotafsiri vibaya agizo la Rais Magufuli kuwa halikumaanisha wafanye biashara kiholela mahala popote bila utaratibu bali wazingatie sheria zilizopo zikiwamo za mipango miji na usafi.

Simbachawene pia amewaagiza wakuu wa mikoa na wilaya pamoja na mamlaka za serikali za mitaa, kuhakikisha wanatekeleza agizo la Rais John Magufuli la kuwatafutia maeneo ya kufanyia biashara wafanyabiashara hao na kuwashirikisha kwenye mchakato mzima wa kubaini maeneo yenye wateja na miundombinu rafiki.
Aidha, watendaji nao wametakiwa kutotumia tafsiri hiyo kususa na kuwaacha wamachinga wafanye biashara zao kiholela.
Amesema endapo utaratibu huo utafuatwa pamoja na mambo mengine utaweza kurasimisha shughuli za wamachinga hali itakayosaidia pia kundi hilo kuchangia mapato ya halmashauri kwa kiasi kikubwa na kuondoa kabisa tabia ya kufukuzana fukuzana kila kukicha.
Hata hivyo, baadhi ya wamachinga katika mtaa maarufu wa biashara wa 'One Way' manispaa ya Dodoma, wamesema zoezi la ushirikishwaji na kubaini maeneo, lizingatiwe vinginevyo wanaweza kugoma endapo watatakiwa kuondoka maeneo hayo na kupelekwa sehemu ambayo haina biashara.

0 maoni:

Post a Comment