Wednesday, December 13, 2017

Rais Magufuli: Amuagiza Waziri wa Fedha kuhakikisha malipo kwa kutumia fedha za kigeni yanadhibitiwa.johnleo

Habari zenu wakuu

Benki ya CRDB inafungua tawi lake jipya mjini Dodoma katika Jengo la LAPF.

Tukio hili liko live TBC1.

Pamoja na wageni wengne yupo Mh. John Pombe Magufuli ambaye ni mgeni rasmi, katibu mkuu wizara ya fedha, mawaziri, spika wa bunge, mkurugenzi wa CRDB DR. Charles kimei na wageni wengne mbalimbali.

Kwa mujibu wa mh. Rais yeye ni miongoni mwa wateja wa CRDB na anaamini CRDB ina mchango mkubwa katika maendeleo ya viwanda na kutoa ajira kwa watanzania.

=======
Rais Magufuli: Amuagiza Waziri wa Fedha kuhakikisha malipo kwa kutumia fedha za kigeni yanadhibitiwa.

> Asema alizuia Mkataba ulioandaliwa na Benki Kuu uliopanga kulipa kwa Dola za Kimarekani. Asisitiza suala hili likiendelea Wasimlaumu.

Rais Magufuli: Pale Benki Kuu(BOT) kuna watu 17 wenye PhD lakini waliruhusu Benki moja kufanya biashara hapa nchini bila kutambua kuwa ni ya kibababishaji.

> Ilipozuiwa Marekani na wao ndio wakashtuka.

Rais Magufuli: Mabeki ambayo hayafanyi vizuri BoT isisite kuyafungia na kuacha mambo ya kubebana bebana

> Ni bora kubaki na beki 5 zinazofanya vizuri kuliko kuwa na benki nyingi zisizo na tija

Rais Magufuli: Najua Makao Makuu yenu yapo Dar lakini nitoa wito kwenu CRDB muangalie utaratibu wa kujenga Makao Makuu hapa Dodoma

> Kwanza itasaidia kutangaza benki yenu na hata mkiwa na jambo mtasaidiwa haraka kwa sababu hata Makao Makuu ya Serikali yatakuwa hapa

0 maoni:

Post a Comment