Saturday, December 9, 2017

Baada ya JPJ Magufuli kuwasamehe babu Seya na familia yake wasanii waguswa na kuandika haya#johnleo

Siku ya December 9, 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli ametangaza msamaha kwa Familia ya Babu Seya, msamaha huo ameutoa wakati wa Maadhimisho ya Miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania bara Mjini Dodoma wakati akihutubia.
Baada ya msamaha huo wa Rais baadhi ya mastaa wameonesha kuguswa na msamaha huo ambapo wameamua kuandika kupitia kurasa zao za Instagram…na baadhi ya mastaa hao ni pamoja na Mchekeshaji Katarina Karatu, Dkt. Cheni, Mh Temba, na Petit Man Wakuache, Afande Sele…
“Mungu ni mwema #salutejpm – Mh. Temba
“Hao uraian Asanteee Rais wangu Mzalendo wewe ndiye Jembe letu mh John Pombe Magufuli Barikiwa sana” – Dkt. Cheni
“Uhuru day pino babaaaaa JPM Tishaaaaa mzee baba” – Petitman Wakuachetz
“Saba mara sabini….Kongole mr president Jpm” – Afande Sele
BREAKING: JPM ameagiza kuachiwa huru kwa Babu Seya na Familia yake

0 maoni:

Post a Comment