Saturday, November 25, 2017

Dr. Lous Shika amefunguka na kusema kwamba amefurahi sana baada ya kusikia kwamba Nyumba za Lugumi ambazoz jana zilifanyiwa mnada wa Marudio zimekosa mnunuzi.#johnleo

 


Dr. Lous Shika amefunguka na kusema kwamba amefurahi sana baada ya kusikia kwamba Nyumba za Lugumi ambazoz jana zilifanyiwa mnada wa Marudio zimekosa mnunuzi.

Dr. Shika ambae alikuwa mshindi wa kuzinunua nyumba hizo kwenye mnada wa awali lakini alishindwa kukamilisha mashrti ya mnada ya kulipa asilimia 25 ya fedha za manunuzi na kusababisha mnada huo kurudiwa tena jana amesema, kukosekana kwa mnunuzi kwenye mnada huo wa marudio imempa nguvu na kusema kwamba ndani ya wiki mbili atafanya mpango wa kuzilipia nyumba hizo.

"baada ya kusikia kwamba nyumba ambazo nimekuwa nikizihitaji kwa muda mrefu kwamba hazijanunuliwa hata mnada wa leo(jana),hiyo mimi imenipa nguvu,nimefurahi"

"Changu ni changu,basi katika wiki mbili hizi zinazofuata   hela itakuwa imeshaingia.Kumbe Mungu amenizunguka bado, yupo pamoja na mimi" .Alisema Dr.Shika


0 maoni:

Post a Comment