Thursday, December 15, 2016

TEAM DIAMOND WAMJIA JUU TUNDA MAN, ADAI AJUTA KISA JAMBO HILI#jphnleo


Msanii wa Bongo Fleva Tunda Man, ambae wiki hii yupo bize kwenye media kwa ajili ya kutoa wimbo wake mpya wa Debe Tupuwimbo ambao ni mzuri sana hata kwa ku-u sikiliza tu, kwani melody na ujumbe uliomo pamoja na Beat kutoka kwa Mensen Selekta kiufupi wimbo uko vizuri.
15403541_175947836207199_3334425051687550976_nTunda Man
Mchongo ni huu ambapo Tunda Man anaonekana kuzingua, ni pale kwenye Cover ya wimbo wake Debe Tupu Kwa mujibu wa madai yaliyotolewa.
Kupitia Cover ya ngoma hiyo ambayo inaonesha Paka akiwa mbele ya kioo na kioo kikimuonesha paka huyo kama Simba, kwa wataalamu wa masuala ya picha za kiuandishi wa habari unaambiwa picha inaongea zaidi ya maneno 1000 sasa kwa Tafsiri hiyo wengi wa mashabiki wa Team Diamond wameona kama kamdhalilisha Simba.
15251602_1638734406427088_3797286551826726912_nKwa maana nyingine Simba ni A.K.Aanayoitumia Diamond Platnumz, so amejitahidi kuwaweka sawa leo kupitia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio, Tunda adai anajuta kuweka ile cover kwani imeleta matusi na maneno ya kebehi mitandaoni na kumfanya akose raha.
“Unajua wakati ile cover inaandaliwa mimi sikuwa Dar nilikuwa Arusha kwenye msiba wa Baba yake na Dongo Janja, so nikawambia waandae so ndiyo wakaweka vile sio kitu cha kushangaza ila nikajuta baada ya kuweka mtandaoni kwani watu wakaanza kufikiria ishu za utimu ila natamani hata niibadilishe niweke hata chui”alisikika Tunda Man akisema.

0 maoni:

Post a Comment