Friday, January 20, 2017

THOMAS ULIMWENGU NAYE KAPATA TIMU ULAYA ASAINIWA MIAKA MIWILI#johnleo


MSHAMBULIAJI wa Tanzania  Thomas Ulimwengu  amesajiliwa na  timu ya Ligi Daraja la Kwanza Nchini Sweden inaitwa Athletic Football Club Eskilstuna kwa mkataba miaka miwili
Baada ya mkataba wake ulimalizika, Ulimwengu  hakutaka kuongeza mkataba mwingine na kusema male go yake ni kutaka kucheza Ulaya.
Ulimwengu alisema: “Kweli nimesajiliwa kwa mkataba wa miaka miwili kuitumikia timu hiyo ambacho nitajiunga nayo hivi karibuni.
“Kwa sasa nashughulikia mambo ya visa kuanzia wiki ijayo  nitaenda nimeshajiunga na timu ya Athletic Football Club Eskilstuna  ya Sweden.”
Ligi hiyo ya daraja la Kwanza inashirikisha timu kumi na nne na inatarajia kutumia vumbi April kumi na nne mwaka huu.

0 maoni:

Post a Comment