Wednesday, March 22, 2017

HABARI | Barnaba afunguka tuhuma za kuachana na mpenzi wake#johnleo

BARNABA AFUNGUKA KUHUSU KUACHANA NA MAMA STEVE

Moja kati ya story ambazo zilikuwa zinakiki kinoma noma wiki chache zilizopita ni pamoja na kuhusu mahusiano ya Mkali wa Bongo Fleva Barnaba Boy na aliyekuwa mpenzi wake Mama Steve.
Ni mengi yaliongelewa kuhusiana na issue hiyo lakini hatukubahatika kupata nafasi ya kuisikia sauti thabiti kutoka kwa Barnaba akizungumzia kuhusiana na issue hiyo.
Leo kwenye XXL ya Clouds FM Barnaba alikuwa na excluisve interview wakati akizindua ngoma yake mpya inayokwenye kwa jina la Lonely.
Na moja kati ya maswali ambayo Barnaba ameulizwa ni pamoja na hilo kuhusiana na mzazi mwenzake, na mkali huyo amemaliza utata wote kwa kusema kwamba ni kweli yeye na Mama watoto wake (Mama Steve) wametofautiana kwa kipindi kirefu sasa.
“Siwezi kusema kwamba tumeachana wala tumetengana, mimi na Mama Steve tumetofautiana, na ni kwa kipindi kirefu sasa.” Alisema Barnaba.

0 maoni:

Post a Comment