KARIBU SANA MSOMAJI WA MAKALA MBALIMBALI KATIKA BLOG YETU(MTEGA BLOG)
MATUMIZI YA BLOG
1.KUWEKA HABARI NA TAARIFA MBALAMBALI.
Unaweza
 kutumia blog yako kuweka au kutangaza habari mbalimbali za 
kikanda,kitaifa au hata za kimataifa.Habari kwa maandishi,Habari kwa 
Picha na Habari kwa Sauti na Habari kwa Video,Chaguo ni lako.
2.KUWEKA TAARIFA ZAKO BINAFSI
Unaweza
 kutumia BLOG kutunzia taarifa zako mbalambali kama vile matukia\o yako 
ya kila siku,taarifa zako za nyumbani n.k ANGALIZO:KAMA UNATAKA UWEKE 
TAARIFA ZA SIRI IWEKE BLOG YAKO KATIKA PRIVATE,Baada ya kufanya hivyo 
hakuna mtu yeyote atakayeweza kuona taarifa zako hata kama akaingia 
katika BLOG YAKO.
3.Kutangaza biashara yako
NDIO,
 Kama una biashara yako na unataka kuinadi kupitia blog basi inawezekana
 kabisa hapa kuna mbinu zinazohitajika ili uweze kufanikiwa katika 
hili.Lugha ya Mvuto,Utumiaji mzuri wa Picha,kuwa Mbunifu na jifunze 
jinsi ya kuongea na wateja.Toa ofa na mengineyo.
4.KUTUMIA BLOG KWA AJILI YA MAWASILIANO KATIKA KAMPUNI
Kivipi,
 unaweza kuitumia blog yako kwa ajili ya mawasiliano ya kampuni au 
Shirika mara nyingi blog za aina hii huwa zinwekewa password hivyo Mtu 
asiyehusika hawezi kuingia.Hata wewe unaweza kufanya pia.
5.Kutumia Blog katika Taasisi Mbalimbali
Unaweza
 pia Kuitumia Blog katika taasisi mbalimbali kama vile 
Shule,Vyuo,Taasisi za kidini na hata Vikundi mbalimbali.Blog itasaidia 
kurahisisha Mawasiliano.Kwa mfano Blog ya Shule inaweza KUTUMIKA kuweka 
taarifa mbalimbali na matukio ya Shule/Chuo kama vile Ratiba ya 
Vikao,Ratiba za Mitihani na mengineyo.Blog ya shule na Chuo pia inaweza 
kutumika kuweka JOINING INSTRUCTIONS(Hii ni barua inayotoa mwongozo wa 
MAELEKEZO Y KUJIUNGA NA CHUO AU SHULE HUSIKA) Kumekuwa na ugumu wa 
kupatikana kwa barua hizi na hivyo kuwafanya wanafunzi MUDA MWINGINE, 
kusafiri umbali mrefu kwenda shuleChuo kuchukua JOINING INSTRUCTIONS 
LETTER,BLOG INAMALIZA TATIZO HILI.
TUNAKUTENGENEZEA BLOG KWA GHARAMA NAFUU KUANZIA TZS 20,000/= TU.
TUPIGIE 0758297744.
ZIFUATAZO NI NJIA AMBAZO UNAWEZA KUZITUMIA KUJIINGIZIA KIPATO KWA KUPITIA BLOG.
Hii
 ni sehemu muhimu ambayo karibu kila anayefungua blog anataka afahamu 
jinsi gani anaweza kuingiza kipato kwa kupitia blog.Swali linakuja je ni
 kweli mtu unaweza ukaingiza fedha kwa kupitia blog? Jibu ni NDIO
 unaweza kuingiza kipato kwa kupitia blog.Kabla ya yote unatakiwa 
ufahamu kuwa fedha ni thamani na thamani yoyote haipatikani pasipo 
kuifanyia kazi,hivyo kuingiza fedha kupitia blog vivo hivyo inahitaji 
ujitoe kwa kweli.Fahamu pia kuwa inahitaji muda hadi uweze kuingiza 
kipato kupitia blog.Urefu wa muda unatofautiana kuna ambao wanaanza 
kjiingizia kipato ndani ya siku kadhaa wengine miezi kadhaa na wengine 
inafikia hadi mwaka au zaidi.Yote haya hutegemea Aina ya BLOG
 na makala zinazowekwa,Kwa mfano ni vigumu kuingiza fedha haraka kama 
utafungua blog ya ktoa taarifa na habari.Hata hivyo ukiwa Mbunifu zaidi 
hakutakuwa na kikwazo.
1.KUWEKA MATANGAZO YA WATU KISHA WAKAKULIPA
Hii
 ni njia namba moja na maarufu sana utakayoweza kuitumia kujiingizia 
kipato kupitia blog yako.Fahamu kuwa kuna wafanyabiashara ambao 
wanatafuta wateja mtandaoni.Ili uweze kumshawishi mtu aweke tangazo lake
 katika blog yako lazima blog yako iwe na vitu vifuatavyo:
i)Lazima blog yako iwe na watembeleaji wengi.
i)Lazima
 blog yako iwe hai(hii ina maana ya kwamba blog yako iwe inawekwa makala
 mara kwa mara,isiwe umeweka makala leo,kisha unakaa mwezi mzima 
haujaweka makala).
2.Kuifanya blog yako iwe ya kulipia
Hii
 ni njia ya pili unayoweza kuitumia kujiingizia kipato kupitia.Faida 
kubwa iliyopo ni kwamba wewe ndiye unaamua nani atazame blog 
yako.Unaweza ukaifunga blog yako na ikawa hakuna mtu anayeweza kuingia 
katika blog yako bila ya wewe kumruhusu.Na utamruhusu pale atakapofanya 
malipo.
KUMBUKA:Ili
 kuweza kutumia njia hii na uweze kufanikiwa katika kujiingizia kipato 
kupitia blog yako ni lazima uandike vitu vya thamani,yaani uandike vitu 
ambavyo vina faida kwa watu,pia viwe vitu ambavyo havipatikani sehemu 
nyingine yoyote bure.Usihofu sio kazi kubwa unachotakiwa kufanya ni 
kujifunza sifa au stadi za blogger aliyebobea.
Blogger=Mtu anayemiliki blog au anayeandika makala katika blog au mwendeshaji wa blog.
Jifunze jinsi ya kuwa Blogger aliyebobea(Mtaalamu).
Zifuatazo
 ni sifa za Blogger aliyebobea(Unatakiwa uwe nazo sifa hizi ili uweze 
kujiingizia kipato kupitia Blog).Usijali sio lazima zote,Anza na chache 
Nyingine Utajifunza Baadae.
i/.Uwezo wa kuandika makala zenye mvuto na zinazoeleweka.
ii/.Uwezo wa kufanya tafiti,Blogger anatakiwa awe na uwezo wa kufanya utafiti juu ya yale anayotaka kuandika.
iii/.Blogger anatakiwa awe na uzoefu na Mitandao tafutaji(Search Engines) .
.Blogger anatakiwa awe na ujuzi wa kuandika kiufasaha.Andika kitu kinachoeleweka.
iv/.Kuwa na Nidhamu katika Blog yako.Weka Makala lkatika blog yako kwa Utaratibu Maalumu.
v/.Ujuzi katika matumizi sahihi ya picha namichoro.Picha na michoro ina umuhimu Mkubwa katika ka kuonngeza mvuto wa Makala.
.
3.Kuweka matangazo ya Google ADsense/Adword.
Unaweza
 kuweka Matangazo kutoka Google /Wordpress na Ukalipwa kutokana na idadi
 ya watembeleaji wa blog yako watakaotembelea Blog hiyo.Kuna sifa za 
kuweza kuruhusiwa kuweka Matangazo ya Google au WordPress.
Hii pia inahitaji blog yako iwe na makala za kutosha na iwe na watembeleaji wakutosha.
4.Kutoa kozi mbalimbali ambazo watu watakuwa tayari kujiunga nakozi hizo NA KUZISOMA KWA MALIPO UTAKAYOWATOZA.Hii
 wala si kazi kubwa ingawa inahitaji muda na kujitoa.Kama una ujuzi 
wowote na unataka kuwafikishia watu kisha wakulipe basi fahamu kuwa 
kupitia blog unaweza kuwafikia watu wengi sana utaifanikisha kazi hii 
kupitia blog yako.Nakushauri kutumia Kiswahili kwani ndiyo lugha ambayo 
watanzania wengi wana umahiri nayo kuliko lugha nyingine.
Ili uweze kufanikisha hili unatakiwa uweke ulinzi(wa password) KATIKA KOZI ZAKO.
5.Kutangaza biashara zako.
Tukiacha
 kutangaza biashara za watu pia wewe mwenyewe unaweza kutangaza biashara
 zako na ukaongeza wateja kupitia blog yako.Hii inajumuisha bidhaa zote 
za mtandaoni na zisizo za mtandaoni.Unaweza kuandika vitabu mbalimbali 
kuanzia vya masomo hadi vya hadithi na kadhalika.Vitabu hivi utaviandika
 kupitia MS Word au program nyingine inayoweza kufanya huduma hiyo na 
utawauzia wateja kwa kuwatumia katika email zao.
Ili
 uweze kupata soko la uaminifu unaweza ukaandika kitabu cha kwanza na 
kukitoa BURE KABISA au kwa Ofa.Usishangae, kufanya hivi kutajenga 
uaminifu mkubwa na kama kitabu chako kitakuwa kizuri basi unaweza kupata
 soko kubwa kwa vitabu utakavyovitunga baadae na kuviuza.
KUONGEZA WATEMBELEAJI KATIKA BLOG YAKO
1.Itangaze Blog yako katika Mitandao ya kijamii,kama vile Facebook,Twitter,Instagram,WhatsApp na kadhalika.
2.Andika makala zenye mvuto na zinazoeleweka.Hii itawafanya watembeleaji wawe wanatembelea mara kwa mara.
3.Itangaze blog yako kwenye mitandao mikubwa yenye watembeleaji wengi.
4.Kuwa
 na utaratibu wa kukomment katika mitandao mikubwa yenye watembeleaji 
wengi.kisha acha link ya blog yako,kwa njia hii unaweza kupata 
watembeleaji,ila jitahidi kukomment kitu chenye maana/thamani.
5.Chukua
 maoni ya wasomaji wako na uyafanyie kazi,hii itawafanya wasomaji wako 
waendelee kutembelea blog yako kwani watakuwa wanakipata 
wanachokitaka.Ukienda kinyume na wasomaji wako ,wanaweza kukukimbia na 
kutafuta blog nyingine itakayowafaa.
6.Weka makala katika blog yako kwa utaratibu maalumu.
7.Andika
 makala za muda mrefu.Makala za muda mrefu zina manufaa makubwa kwani 
hatakama makala uliiandika mwaka uliopita bado itakuwa na thamani.Na 
watu wataendelea kuisoma kwani bado ujumbe unatumika.Makala za habari 
zinadumu kwa muda mfupi sana.
8.Kuwa
 mbunifu ifanye blog yako iwe ya kuvutia,Buni Mwonekano wa blog yako uwe
 wa kuvutia,kuna rangi nyingine Ukiweka unafukuza watembeleaji(Color 
Psychology).
9.Kichwa cha makala kinachovutia.
Jitahidi kuandika kighwa cha makala kinachovutia ili umshawishi MSOMAJI Kuendelea kusoma.
10.Watambue wasomaji wa Blog yako.
Ni vema uwe na wasomaji 10 wa blog yako unaowatambua,kuliko kuwa na wasomaji 100 usiowatambua.
Ninapozungumzia
 kufanikiwa kupitia BLOG yako wengi wanweza wakapeleka mawazo yao katika
 UCHUMI,HASHA sina maaan hiyo,bali ninachikusudia hapa ni jinsi gani 
unaweza kufanikiwa katika blog yako.Hii ni kwa sababu watu walio wengi 
hawadumu katika blog zao ,yaani mtu akifungua blog baada ya muda mfupi 
tu miezi kadhaa(na wengine hata siku kadhaa) HIVYO mtu wa aina hii 
ameshindwa kufanikiwa katika blog yake.
Zifuatzo ni sababu zinazowafanya Watu wengi washindwe kufanikiwa kupitia blog zao.
1.Kiwewe cha BLOG.
Nini
 maana ya kiwewe cha blog? Kiwewe cha Blog ni hali ya mtu kutamani sana 
awe na(amiliki) blog,na kufikiria kuwa ni kazi rahisi sana,Ukweli ni 
kwamba KUTENGENEZA BLOG ni kazi rahisi sana,tatizo linakuja katika jinsi
 ya kuiendesha.Inahitaji nidhamu ya hali ya juu sana la sivyo safari 
yako ya blog itaishia njiani.Sababu hii huwafanya wengi waachilie mbali 
kuhusu blog na hivyo kushindwa kufikia malengo.
2.UTIAJI Chumvi wa baadhi ya watu katika Matangazo yaao ya kujinadi.
Kuna
 baadhi ya watu wanatia chumvi sana kiasi kwamba inaonekana kuwa 
kutengeneza/kujiingizia fedha kupitia blog ni kama kazi ya saa moja 
tu.Mfano unaweza ukakuta tangazo linalosomeka ‘’FUNGUA BLOG LEO UANZE 
KUPOKEA FEDHA’’ au “FUNGUA BLOG LEO UANZE KUINGIZA KIPATO CHA MAANA,SI 
AJABU WENGINE WANAFIKIA HATA KUSEMA UWE TAJIRI’’.Matangazo ya namna hii 
na kwa mtu mwenye uelewa wa chini anayachukulia kama yalivyo.Pia 
wanashindwa kufahamu kuwa hiyo ni Lugha ya kibiashara tu.SI UONGO BLOG 
inaweza kukufikisha KWENYE UTAJIRI Lakini si kwa haraka na kiurahisi 
namna hiyo.Watu wa namna hii mara nyingi huishia kufunguia blog tu na 
kuiacha kwani anakuta mambo tofauti na vile alivyoambiwa.
3.KUKOSA CHA KUANDIKA
Wapo wanaoshindwa kupata cha Kuandika,na hivyo huishia kati katika safari yao ya Blog.
>>>SULUHISHO:Hakuna
 kitu kipya Duniani usiogope kuona hakuna kipya,utakachoandika kwa kuona
 kila kitu kimeshaandikwa.Andika tofauti na Wenzako,kuwa Mbunifu na hii 
ndio faida ya kufanya utafiti kwani utafahamu mapungufu ya wengine 
katika makala zao na utajua jinsi gani utayarekebisha kupitia makala 
zako mpya utakazoandika.
PIA,Jijengee
 utaratibu wa kujisomea Soma Vitu Mbalimbali vitakavyokuongezea 
Maarifa.Soma mtandaoni,soma vitabu,soma magazeti n.k.Ukijijengea 
utaratibu wa kujisomea utaongeza maarifa ya kutosha yatakayokuwezesha 
kupata makala za kuandika,sio kucopy.
4.KUTOKUWA WAVUMILIVU
Kuifanya
 Blog yako iwe chanzo cha mapato inahitaji Muda wa kutosha.Sio rahisi 
kuanza kufungua Blog leo na kesho ukaanza kupokea fedha.Kutokana na hali
 hii watu wasiokuwa wavumilivu huamua kuachana na Blog.
>>>SULUHISHO:Inahitaji kuwa Mvumilivu ili uweze kufanikiwa katika blog yako.Kuwa Mvumilivu na tumia mbinu mbalimbali kuiboresha blog yako.
5.KUTOPATA WATEMBELEAJI
Kupata
 Watembeleaji katika Blog yako inategemea vitu vingi.Kuna watu 
wanapofungua blog na kuona hakuna watembeleaji huamua kuachana na blog.
>>>>SULUHISHO:Ili kuongeza Watembeleaji katika blog yako Tumia mbinu zifuatazo.
*UNAHITAJI USHAURI KUHUSU BLOG YAKO TUANDIKIE(BURE!!)
E-Mail:godfreymtega@gmail.com
"TUTAKUTENGENEZEA APPLICATION YA ANDROID YA BLOG YAKO"
TUNAKUTENGENEZEA BLOG KWA GHARAMA NAFUU KUANZIA TZS 20,000/= TU
TUPIGIE :0758297744(whatsapp)/0716824009

 
 
 
 
 
 
 
0 maoni:
Post a Comment